Waso haya wana Mji Wao. 002. (Mke Wa Mtu Sumu).

Mmmmmh… Mambo mengine ni mazito kusimulia , ila itatubidi tuambizane , huenda ikawa sababu ya kumuokoa mtu, la! Mtu itakuwa ni kwa uchache mno, liwaokoe watu, maana wapo wengi waliolivalia njuga na kukosa haya. Dunia imepasuka mahali kama wasemwavyo wengine, Nani ataziba kiraka au kama ni ufa halikadhalika? Maana, usipoziba ufa utajenga ukuta.Wapo wengine walosema, wameabiri basi la dunia lakini lipo kasi mno, wakamrai konda na dereva wakiegesha sehemu , wawashushe ! Maana dunia iko kasi mno. Fikra zao zinawapa taswira ya dunia jinsi ilivyo, sijui mimi na wewe tunaiwazia nini au kuchelea lipi katika safari yetu ya maisha na hatima yake. Kilele kitafika na tutaiaga dunia, Hilo halina shaka, lakini kwa sasa hivi tutaishije? Wahenga walisema, ukiishi na Mtu wa bunduki, utakufa na Mtutu wa bunduki, hivyo basi ni bora kubadili mienendo kabla hayajakukuta ya kukuta. Kama asemavyo msanii mmmoja wa kuchekesha kule Tanzania kwa jina la Tabu Mtingita, ‘ Aaasubuutu..kitamkuta Mtu kitu hapa, anakufa mmoja wallahi, umetindinganya mambo, ungenisikiliza , usingeyatondomoa (usingeyaharibu).’

Sasa hebu tega sikio, macho yakodoe kodo, akili yako, nafsi, hisia zako zote pamoja na kiwiliwili ziandamane nami. “Mke wa Mtu Sumu” Ni kauli inayosemwa mno , imezoeleka sana , mpaka watu wanaichukulia ni ya kawaida mno. Sisi vijana husema kwa dhihaka, ‘kama mke wa mtu sumu tutamnywa na maziwa’ , yaani sumu kiboko yake maziwa, ndio huduma ya kwanza kwa mtu aliyekunywa Sumu. Lakini wengi wanakosea mno, sio kila neno linalosemwa lina haki ya kulidhihaki, mengine iko haja ushike sikio na kujiuliza maswali mengi, uwatake wakubwa na ushauri na ulipe jambo Hilo mazingatio.

Maana yake kubwa msemo huu ni; Haifai kwa mtu kutembea na mwanamke wa mtu ambaye ameolewa kisheria. Bibilia imeandika, ‘Mwanamke mpumbavu huivunja ndoa yake kwa mikono yake mwenyewe.’ Lakini haikunuia kumuelimisha au kumuonya mwanamke pekee, hata mwanamume mpumbavu halikadhalika huvunja ndoa yake kwa mikono yake mwenyewe. Zinaa ya watu walio katika ndoa ina uzito mkubwa mno, ndio maana hata katika Kitabu cha Korani tukufu, hukmu iliyotolewa na Mungu kwa Vijana ambao hawajaoa wanapofanya tendo la zinaa , ni kupigwa bakora themanini, ilhali kwa wale wanandoa wanapozini, hukmu Yao ni kupigwa mawe mpaka kufa , hukumu nzito, kwa uzito wa jambo lenyewe. Dhambi inapokithiri , watu hutaka kuhalalisha yaliyoharamishwa na kuyafanya yaonekane kawaida, ilhali ni kinyume na uhalisia wa mambo.

Wapo wanawake wengi ambao japo wameolewa , huwaendea kinyume waume zao na kutoka ndani ya ndoa Hadi kufanya mapenzi na wanaume tofauti na wale waliowaoa, cha kushangaza zaidi, wengi wao utawakuta wameivua Pete wakificha wasijulikane kwamba ni wake za watu. Wanajitongozesha na kuapa kabisa kwamba hawajaolewa, ama kutoa Siri za chumbani kutafuta sababu za kufanya uchafu na kutembea na wanaume wengine.

Wanaume wanapenda na kujawa na matanio tu kwa kumuona mwanamke, anapomuuliza mwanamke na akakiri kwamba hajaolewa ni rahisi kwake kujenga mahusiano ya kimapenzi nae iwapo ametokea kumpenda au kutamani muonekano wa mwanamke huyo, unafahamu fika hasi na chanya Ndizo zinazoungama, ukimuekea mbuzi nyasi azilinde, ukija zimeliwa wala usimuulize zimekwenda wapi. Na vilevile Wapo aina ya wanaume na vijana wanaojitapa kifua, kwa kutaka kutembea na wake za watu , hawatongozi ila wanawake ambao wameshaolewa , wakijidai ndio mafundi wanaokarabati wafikishe magari mbele ya safari ambako pengine walioko katika ndoa hawafiki.

Wala hili siliamini, ni ufuska tu uliojikita katika nyoyo za watu, wamejizoeza tabia chafu, ni watu aina yake lakini, wana mshipa flani wa uzinzi ndani Yao, wewe mwanamke unataka nini zaidi ya stara uliyoipata katika ndoa? Vipi uzurure ukijinadi kwamba hujaolewa ilhali ni Mke wa mtu? Watu wamekosa haya, na ndio maana wengi wanatembea barabarani nusu uchi wala habari hawana. Kwa hali hii tunataraji tukimuomba Mungu atusikie? Na pia atuepushe na majanga kama hili janga la maradhi ambukizi ya Corona?

Dhambi zikikithiri ndio maisha yanakuwa magumu mno na wanadamu tunanyanyasika , hebu turudini kwa Mungu na tubadili tabia zetu. Majuzi kuna bwana mmoja alifanyiwa Kitendo cha unyama mno ambacho wala hakisemeki, kinakirisha mno, na visa vingi kama hivyo vimefanywa kwa watu wanaotembea na wake za wenyewe. Kijana mwenzangu, au mwanaume mwenzangu, iwapo mwanamke yuko katika ndoa na hajiheshimu, ni jukumu Lako wewe kuwa imara na kumuepeka , kutokuwa na mahusiano yoyote ya kimapenzi.

Wanasema malipo ni hapa duniani, na dhambi la zinaa linalipa hadi vizazi saba vya ukoo wa mtu. Ukitembea na mke wa mtu ukajiona kidume, amini utalipwa na mkeo, au mwanao, mamako, Shangazi yako, dadako, mjukuu wako, almuradi aibu ikufike ujihisi uchungu kama alivyohisi huyu uliyetembea na mkewe. Mke yu uchungu, kweli sikatai, na anauma mno achukuliwapo na mwengine na mwenyewe ukeli hai, hukutia majonzi ukawa hujifai, usipokuwa makini ukazirai, na maishani ukakosa kufurahi. Wanaume wengi wanapojua kwamba wake zao wanawaendea kinyume huwapa talaka na kubaditilisha ndoa, wengine huwapiga wanawake nusura kuwaua, wengine kwa kushindwa kujizuia wakawaua wake zao na watoto na kujiua wao wenyewe pia, zote ni hasira za mke kutoka nje ya ndoa. Mtu hufikiria Mali alizotoa na Fadhila alizompa mwanamke huyo ndani ya ndoa kama Mzazi mwenzake akashindwa kuelewa chanzo cha kukosewa kiasi kikubwa mno.

Majuzi kijana mmoja alietembea na mke wa mtu mara si moja alifuatwa na mume wa Yule mwanamke aliyetembea nae,alikuwa yupo kwenye stendi anapofanya kazi yake ya bodaboda, baada ya mazungumzo ya muda kuhojiwa kuhusu kutembea na mke wa Yule bwana, kijana alikana, lakini baada ya kutishwa, kushurutishwa na kuonyeshwa hadi ushahidi wa picha na meseji kwenye simu ya mwanamke Yule, kijana hakuwa na budi kukubali. Kwa ustaarabu yule mdhulumiwa akamuomba waondoke sehemu kando kidogo ambapo wangekwenda kuongea na kuelewana au la sivyo amuanzishie mtiti palepale na aieleze halaiki kuwa kijana huyo alikuwa anatembea na mkewe, kwa hali hio hata ukitiliwa na kelele ya Mwizi watu watakuvamia, kukufakamia juu kwa juu,na kukupiga kitutu kama Mbwa aliyeingia msikitini, ilimradi wakunyooshe na kukutia adabu ili usirudie kosa lako. Basi kwa uamuzi wa busara kijana aliongozana na bwana aliyekuwa akimla uroda mkewe ambaye alihitaji faragha Yao wawili. Walipofika katika jengo alioelekezwa , mijanadume kama Tisa ilitokeza na kumkamata akashindwa kujitetea, watu hao wakamfanya mwanamke au wakamuingilia ambapo Hilo ni kinyume na maumbile, kijana akapiga kelele bila msaada wowote ila baadae wakaja kumsaidia kutoka katika sehemu ile aliyokuwa.

Kwa kisa hiki nilijifunza mengi, kikanichukiza mno, haijuzu kulipa ubaya kwa ubaya, makosa mawili hayatengenezi walau jema moja, halafu hili lilikuwa dhambi kubwa mno. Tumesikia watu wamekwama na kugoma kutoka katika tendo la ndoa baada ya kutembea na mke wa mtu, wengine wakawekewa tego na kubaki na uvimbe katika sehemu zao za korodani, na Kuwa na mapumbu , au wengine wakarogwa na wanaume wenzao na kuwa wendawazimu , au kufanya mashine zikate moto, au hata kuuwawa kwa kutembea na mke wa mtu.

Hizi ndio Zile Sumu tunazoambiwa; ‘Mke wa mtu sumu.’ Hebu tuweni na staha na tujitathmini, kufanya kosa si kosa, lakini kurudia kosa ndio kosa, Leo tuakifike na wake za watu, naamini kama walivyosema wahenga; Mui huwa mwema. Tubadilisheni mieneno na tuweni bora wa tabia. Ama kwa hakika; Mke wa mtu siku zote atabaki kuwa sumu.

Wazazi Tuwatende Hisani(Wema).

Nilikuwa naelekea msikitini ‘msikiti mdogo‘ kama walivyoufahamu wengi katika mtaa wa Magaoni, Tanga , kuswali swala ya Adhuhuri huku nimeandamana na kakangu Shamuni na walimu wengine. Ulikuwa ndio msikiti uliokuwa karibu zaidi na shuleni tulipofanya kazi. Tukalipita duka la Bajaa na kukunja na barabara ya mchanga iliyokwenda moja kwa moja hadi msikitini.

Jua lilikuwa Utosini, ni saa saba kasorobo , Linachoma si haba, ndio pwani ilivyo siku zote, joto lisoyumkinika.Karibu na msikiti pana nyumba iliyojengwa takriban miaka kumi iliopita ila haikuezekwa, imebaki mahame au gofu, mawe yaliyotumiwa kujenga yametanda weusi kwa kukaa muda mrefu, lakini nyumba hii hulimiwa na kufanyiwa usafi kwenye mazingira yanayoizunguka, ishara ya kwamba pengine haijasahaulika na tumaini na nia ya kumaliza ujenzi upo. Nisikwambie mengi nikaishilia kutia chumvi, hata mwenyewe sikumfahamu.

Nje ya jengo hilo kulikuwa na Nyasi ndefu na mimea mingine iliokua, Bi. Kizee wa takriban miaka sitini na tano hadi sabini na… analima na kupalilia magugu ishara ya kusafisha mazingira na kuandaa sehemu ya kupanda mazao kwani alikuwa amepiga mchanga matuta, na awali niliona maharage Yakiwa yanakuzwa sehemu hii. Mwenyewe Bibi kajichokea si haba, umri umekwenda ila hana budi kushika jembe alime angaa huenda akapata chakula baada ya kupanda mazao na kuvuna.

Tuliingia msikitini na kusali , kisha tulipotoka tukakaa kwenye baraza ya nyumba kando na nyumba iliyo mahame ambapo kando yake ndipo Bibi alikuwa anashughulika. Dukuduku likanijaa moyoni, moyoni ukashindwa kuvumilia nikaliona kooni, baada ya kutafakari nikamuuliza mwenzangu, ‘Hivi Yule mama mtu mzima anafanya kazi katika jua kali namna hii huku akionyesha kuteseka kabisa na kazi ile ya sulubu, kwani hana mwanae mwenye nguvu ambaye angemsaidia ?’

Akanijibu; ‘Huenda anae mtoto na wala sio mmoja, ila watoto wengi wamekuwa wakaidi na wakorofi kiasi cha kuwaacha wazazi wao wataabike.’ Nikakumbuka maneno yanayosemwa kuhusu watu ama watoto wanaofaulu kimaisha, wakakaa mjini na kusherehekea alivyowatunuku Mungu ,kwa kukata na kula minofu wakiwasahau wazazi wao wakiteseka vijijini.

Mungu amehimiza wanadamu katika vitabu vitukufu kama korani, kwamba ‘Muabuduni MwenyeziMungu na Wafanyieni wema wazazi wawili.’ Na vilevile mseme, Ewe Mola wetu tusamehe sisi na wazazi wetu, na uwarehemu kama walivyotuhurumia sisi tukiwa wadogo au wachanga.’ Kwa hivyo , Mungu anatuelekeza kwamba jambo la kuwatendea wema wazazi ni la muhimu mno, ukiwa uhusiano wako mwema na Mungu basi upatilize na uhusiano mwema na wazazi wako, ndio utakuwa umepata kufaulu.

Lakini ni masikito makubwa kwamba baada ya wazazi kutulea, kutusomesha, kutujenga, na kupambana tupate maisha mazuri , huwa tunawasahau na kuwatenga. Wako vijijini wanateseka, wale mihogo na mboga za majani kwa wingi, sio kwamba eti si chakula, ila wakosa kula vyakula bora zaidi, watamani pilau, Kuku, wali na minofu mingine eti mpaka siku ya kuja wewe nyumbani, hivi kweli unawapenda, katika umri wao ulioenda ushindwe kuwaandikia mtu wa kuwasaidia kazi za nyumbani kama kufua na kupasi, kupika na hata shughuli za usafi wa mazingira na kilimo, wasulubike na majembe kumaliza nguvu zilizobaki mwilini?

Inakua haimpendezi Mungu, nikajihisi niwaase na vijana wenzangu, hebu tuwahurumieni wazazi wetu mno, Tupambane na michakato yetu ya hali , na iwapo tutajaaliwa kupata tuwakumbuke waliotuleta duniani, Nina Imani wakidumu katika Furaha na kutokupungukiwa , Furaha Yao ndio zao la baraka nyingi kwetu kutoka kwa Mungu. Tuwafanyieni wema , na kuwahurumia wazazi, wala tusiwabughudhi na kuwaudhi muda wote, wema wa mzazi huwezi kuulipa kwa namna yeyote , lakini tuirudishe Imani Yao na mkono wa hisani kwa kutulea kwao na mapenzi waliyotupa.

WASO HAYA WANA MJI WAO. 01.

Kweli , thamani ya mwanadamu iko kwenye utu na wala sio vitu. Lakini iweje mwanadamu aishi kama hayani? Puh! Ama niseme hayawani pia ana ubora fulani, haiyumkiniki lakini ndivyo maisha yalivyo sasa hivi. Ukitaka kuleta usawa ama uungwana katika hii dunia ya sasa, utaonekana mshamba aliyeishi karne za jiwe kabla ya uvumbuzi wa chuma. Masikitiko makubwa kwamba, yasiyopendeza na kuwa kinyume yamekuwa kawaida, si wakubwa wala wadogo , wote wameangamia.

Utovu wa nidhamu na ufuska umetawala. Leo kuvaa na kutembea nusu uchi ni kawaida, eti wanasingizia ni fasheni, mitindo inayokwenda na wakati wanasema. Heri ya wale wanaomkumbuka Mungu na kutuasa kwamba tunaishi katika nyakati za mwisho, si kitambo, jamvi la dunia litakunjwa na mwenyewe Manani. Na kwa jinsi hali zilivyo, wanasema alama za awali za kiyama ama kuondoka duniani zimedhihiri.

Hivi ni mwanadamu gani mwenye akili razini , anapiga picha uchi wa mnyama na kuzianika mtandaoni, ukiulizwa utaambiwa ni modo (Model), socialite ama Mwanafasheni, Mimi hupita humo katika mitandao ya kijamii , si Facebook, Instagram, YouTube na Mingine mingi, mda mwingine macho yanajikodoa nusura yatoke .

Stara imekosekana, vilevile nisifahamike kimakosa, mitandao ina faida zake lukuki tu, lakini yuko wapi wa kuwaeleza watu wajitenge na mambo ya kipuuzi yasiyoweza kuwanufaisha kwa lolote? Watoto wanapewa simu na iwapo sio chini ya uangalizi wanapata fursa ya kuona picha hizo chafu zisizoridhisha, au hata kanda za ngono zilizorekodiwa mitandaoni, ndio kila kukicha walimu wanafunza na kuwaelekeza lakini yanaangia na upande mmoja wa sikio na kutokea sikio jingine, watashika saa ngapi iwapo vichwa vimejaa mambo yasiyo na msingi. Wasanii haswa waimbaji wa nyimbo za kizazi kipya wanakaidi kanuni za sanaa, Sanaa ni njia mojawapo ya wanajamii kueleza hisia zao na kutoa dukuduku Lao, kama katika ushairi, uandishi na tungo nyingine mbali mbali.

Ni kweli msanii haandiki kutoka nafasi hewani, ila mawazo yake yote ni athari ya mazingira yanayomzunguka, matukio aliyopitia na muingiliano wake na jamii kwa ujumla. Hii ndio sababu msanii akaitwa kioo cha jamii. Nyimbo za zamani zilikuwa na mvuto na maneno yenye hekima nyingi na yenye kuelimisha jamii, Leo mziki wa kizazi kipya kando na ule wa dini, umejawa na uchafu mwingi, video za muziki zinazoenyesha Dada zetu wakicheza nusu uchi , na maneno ya Kubomoa maadili ya jamii, yenye kuwashajiisha vijana, katika uzinzi, ubakaji, na matumizi ya dawa za kulevya.

Tumeelezwa Mara si moja kwamba , vijana ndio nguvukazi na uti wa mgongo wa maendeleo ya taifa, Leo vijana wengi hawana mwelekeo wanawaiga waimbaji kwani ndio walio na ushawishi mkubwa katika jamii , lakini je! Ushawishi huo unawapeleka wapi? Kwenye manufaa au kwenye kukosekewa. Sanaa hasa uimbaji imekuwa sehemu ya kipato kwa vijana na kuwatoa wengine katika Lindi la umaskini, na kuwasaidia wasiojiweza katika miradi tofauti, lakini ni bora kwa wasanii wetu kujikita katika tungo zinazokuwa maadili katika jamii. Niliambiwa kua uje uyaone, nikafikiri ni maembe, kumbe ni haya maisha ; Baba na mwanae wa kike wa miaka kumi na mitano washiriki ngono na kurusha kanda ya tukio Hilo mitandaoni, Mtoto wa miaka minne abakwa, Mzazi amlawiti mwanawe kwa miaka minne na kuhukumiwa kifungo cha miaka thelathini jela. Majambazi wamvamia mfugaji na kumuua kisha kuondoka na ng’ombe zake kumi, miongoni mwa habari zinazopenya maskioni kupitia vyombo ya habari, mambo mazito yasiyoleta furaha yoyote.

Mapenzi ya mali yametufikisha pabaya, watu wanaingia katika makundi ya kishetani ili nao wapate utajiri, kinachofuata ni kuwatoa kafara wazazi, ndugu , watoto, kutoa kizazi, kugeuzwa wanawake na kufanya kila linalomchukiza Mungu kwa ajili tu ya kupata mali. Wengine wanawaingilia na kuwaharibu watoto wa kiume kwa Imani ya kupata mali ili wafaulu. Wewe mwanamke uliyeolewa mbona hujawa na staha ukatulia katika ndoa yako? Vijana mke wa mtu ni Sumu, usidhihaki kwamba utakunywa maziwa, usijione kidume kuvuna alipowekeza mwenzio, utaambulia hasara kubwa. Kisha cha kusikitisha kimetokea majuzi, baada ya kijana kutembea na mke wa mtu kwa Mara kadhaa, aligunduliwa na kisha kutendewa uchafu na wanaume sita kwa kumtia adhabu juu ya kumchezea mke wa mtu, dunia ilipofika, naona isimame nishuke, Safari imenichosha na kunichusha , mbele hakutamaniki na nyuma hakurudiki , matukio ya kutisha yako njenje, ni bora kumrudia Mungu na kumtaka msamaha na muongozo, pasi na kushikilia janjajanja na kukithiri makosani.

Fadhakkir.

Merits of the Soul: Struggle against the Self (Jihad al-Nafs)

A brief text about the greatest jihad: the struggle against one’s self.

Struggle against the Self (Jihad al-Nafs)

… By the soul and (by) Him who made it perfect, and then inspired it to understand what is wrong and what is right for it. Truly is successful the one who purifies (his soul). (Holy Qur’an, 91: 7-9)

Imam Ja’far al‑Sadiq (a) said: “The Prophet (s) of God dispatched a contingent of the army (to the battlefront). Upon their (successful) return, he (s) said: ‘Blessed are those who have performed the minor jihad and have yet to perform the major jihad.’ When asked, ‘What is the major jihad?’ the Prophet (s) replied: ‘The jihad of the self (struggle against self)’”. [Al-Majlisi, Bihar al-Anwar, vol. 19, p. 182, hadith no. 31]

A human’s soul is the scene of a struggle of two competing powers. Divine power attracts him towards heavenly spheres, and inspires him to acts of goodness. Satanic power tempts him towards realms of darkness and shame, and invites him to acts of evil. When the divine forces are victorious, a person emerges as a virtuous and blessed being, in the company of prophets, saints, and the pious. When, however, the satanic forces dominate, the person becomes rebellious and vicious and is grouped with infidels, oppressors, wrongdoers and those who are cursed.

What is the struggle against the self?

Jihad al-nafs is the struggle against evil ideas, desires and powers of lust, anger, and insatiable imagination, placing all of them under the dictates of reason and faith in obedience to God’s commands, and finally, purging all satanic ideas and influences from one’s soul.

This struggle is considered as the major struggle (al-jihad al-akbar) as it is much more difficult than fighting in the battlefield, for in the struggle against the self, one has to constantly battle enemies that are hosted inside his own existence.

Islamic ethical teachings indicate that the one who succeeds in this struggle can rise above and beyond the level of angels, and one who fails in this struggle will descend to a level lower than the level of animals, and may even be grouped among the legions of the devil.

The steps of struggle against the self

• Step 1: Reflection: One must devote some time every day to contemplate about his duties towards God, Who brought him into this world, bestowed him with a sound body and brain, and equipped him with intellect and capabilities, all of which are sources of pleasure and joy in his life. God also sent prophets and His Holy Book as a means of guidance and salvation. The aim of this life and purpose of all these blessings is more noble than to follow mundane desires and evil tendencies that are short lived and temporary.

Death may come knocking at any time. This world is a place of doing good actions that result in permanent joy and take one into a higher sphere of existence. A person should therefore reflect on his destiny and his helplessness at the hands of time and age that are passing. He should feel regret before God for the loss of precious years of life and for past deeds that will bring him shame on the day of judgement. He should then begin his struggle to rise above this state of wretchedness and ask God for help to bless him with hope, sincerity, and strength to fight against satanic tendencies and evil traits of character, and to rise beyond material pleasures and worldly gains.

• Step 2: Will and resolve: Firm resolve is the essence of humanity and basic requirement to attain freedom from the domination of evil desires. The will that is required at this stage is synonymous with laying the foundation of a good life. The warrior in this battle of the self should purge himself from sins, perform all obligatory (wajib) acts, make an intention to compensate for the days lost (in sinfulness), and finally, resolve to behave as a rational religious person and a real human being. His manners should be an imitation of the Prophet’s life, and he should follow the Prophet (s) in all his abstinences and choices. All this cannot be achieved unless he learns the laws of Shari`ah and follows them faithfully.

• Step 3: Self-examination, evaluation and criticism: After making a vow to be a person of strong will‑power and resolution, he must understand that the hereafter is the place where his secrets will be exposed. Thus he should evaluate himself on a daily basis to get rid of evil habits and desires, to acquire more noble human character, and to perform better actions than before. He must realize that committing sin takes away from him noble essence of humanity and he must pray to God for His assistance and for the intercession of the Prophet (s) and the members of his Household (a).

• Step 4: Self‑conditioning: The resolve and self-evaluation from the previous steps should form themselves into specific commitments to self-conditioning. For example, one who has an evil habit of lustful eyes, backbiting tongue, or inflated ego should say to himself, “I will not violate the Law of God today” and consciously avoid such habits for one day. By performing such an experiment with sincerity and resolve, he will realize how easy this task is. He should ignore Satan and the evil ideas that will magnify this small task as being difficult or even impossible. Thus, gradually, he can extend this period by experiment and see how easy it is to get rid of an evil habit or to acquire a positive merit.

• Step 5: Guarding against evil: A personstruggling against his own self should constantly concentrate upon his intentions. If any time the idea of violating divine commands occurs to him, he should know that this idea has been instilled into his mind by Satan and his allies, who want to deter him from his good resolution. He ought to curse them, seek God’s compassionate protection, and banish those evil ideas from the realm of his heart. He should reply to Satan that this day also he has to abide by the condition imposed upon his own self that he will not go against God’s commands. Thus with the help of God, Satan will be driven away.

One must remain in this same state of mind until night ‑ the time for self-examination and evaluation of his deeds of the whole day. This is the time to see whether he has been honest to his Creator. If he has been faithful to God, he should be thankful to Him. Such a person has gone a step forward in His direction and became an object of His attention. God will thus continue to help him in performing all worldly and religious duties, and will diminish his pains of struggle in the next day.

And if he repeats this exercise many times, he will be accustomed to acts of piety and the eradication of evil traits. He will observe that it does not require overly cumbersome efforts and obedience to God will give him abundant spiritual pleasure. God forbid, if there are any lapses on his part, he must ask God’s forgiveness, and sincerely implore Him that he will be more careful in future. The Merciful God will throw open the doors of grace and compassion to him, and will guide him to the straight path.

• Step 6: Remembrance: During the whole journey of struggle against self, one should constantly remember God and the graces bestowed by Him. He must at each step, thank Him constantly for His help, mercy, and guidance in fulfilling his intentions. The degree of gratitude to God should increase as he attains a higher stage in his struggle against self. He must realize that it was because of God’s help and response to sincere prayers that he was able to get rid of Satan and his allies from the domain of his heart and attain sublime human attributes loved by God. [adapted from Al-Khomeini, Forty Hadith, ch. 1, ‘Jihad al- Nafs’]

Advice to awaken for the struggle against the self

• It is human nature to thank one who has been gracious. Reflect and estimate the seen and unseen favours bestowed on us by the Almighty. All of the creations of God could not even provide a fraction of such bounty.

• Look at the air we breathe day and night, and upon which our existence as well as that of other living beings is dependent. Nothing can remain alive if it is deprived of such air for even a few minutes. What a marvelous gift of God it is! If all men of the world laboured together to create such a gift, they could not do so. In the same way, reflect on other gifts of God such as the external bodily senses of sight, hearing, taste, smell, and touch, and inner faculties such as thinking, imagination, and reason, each one of which carries unlimited benefits and which is granted to us by Our Lord.

He is the Creator and King of this vast universe. Human being, a creature crawling on one of the smallest planets miserably fails to grasp the extent of his own small world, whose sun cannot even be compared with far greater suns of innumerable galaxies. Our solar system is nothing compared to several other solar systems, which still elude the powerful telescopes of great explorers and investigators. Look at the human brain—what a fascinating creation it is! Can the combined efforts of all human beings make even a single living neuron (brain cell) that Almighty God has created and creates all the time! Surely this God-given brain deserves to be solely the seat of divinely inspired good ideas and not evil thoughts!

• Every living being in this Universe is within the range of His divine vision, so remember God and all His favours, and don’t disobey Him. He fulfils all our needs without having any need of our adoration. Whether you observe His commands or transgress them makes no difference to Him. It is for the sake of our own benefit that He has enjoined good and forbidden indecency.

Overpower satanic ideas and convert the spheres of your mind into divine realm by driving out the evil forces and inviting the divine hosts, so that God may help and protect you in the dangers threatening to befall you in this battle. Do not have any expectations from anyone but God. With all humility and all the tears your eyes can offer, pray to God and seek His assistance to emerge victorious in this crucial battle against the self.

Conclusion

• Imam Ali (a) said: “One who struggles against himself so as to obey God, in the eyes of God, his station is that of a pious martyr.” [Al-Amidi, Ghurar ul Hikam wa Durar ul Kalim, hadith # 3546]

TOPIC TAGS:

CATEGORY:

Comments

ALI KHAN MON, 08/03/2015 – 11:39

Excellent Article.

SYEDA R

NACHELEA UJANA.

Kinywa kweli ni karakana ya maneno, hivi ipo siku umewahi kukaa

chini ukajiuliza kwa siku kinywa kinaweza kutoa takriban idadi gani ya maneno ? Pengine utadhani ni swali la kipuuzi ; lakini kaa ulitafakari. Mimi sio mwanasayansi pengine ukadhani nimelifanyia utafiti ; imenijia katika fikra na nikaona ni aula kukuhusisha na wewe msomaji. Wanasema ,ujana ni moshi ukienda haurudi. Ni umri kabla ya uzee ; takriban ; kubaleghe kwa mwanadamu mpaka anapoingia miaka arobaini. Ni uwanja wa sokomoko ; bughudhi, majivuno na safari ya kujitambua; na hata ukimuuliza yule aliyetulizana katika mashababi ; hatakosa la kukwambia kuhusu uzito wa umri huu. Wazee wangepiga kumbukizi za jinsi walivyokuwa ; Lakini zao zikabaki kuwa zilizopendwa. Kijana hutaka afanye kila analolitaka , pasi na kuingiliwa na Mtu. Ni umri ambao mwili humsisimka mtu; ajione ndio bora zaidi au mbabe. Damu inachemka ; kijana wa kiume asifiwe kuwa kijogoo; anawika mtaani hadi kijijini , awe na ubavu ; hakuna asoweza kupigana nae ; yupo tayari kwa lolote hata kufa . Mengi yaliyo muhimu hushikwa na wachache tu , wasiokuwa na msimamo husombwa na mafuriko ya kutaka kupokelewa na kukubalika kwa vitendo vya wanarika wenzao. Ambaye hajawahi kutumia mihadarati ; aanze kwa sigara ; imkohoze achekwe ; na kisha maswahiba wampe moyo kwamba ndio kukua na kuona upeo wa maisha. Mwisho aivute na kuwa mraibu ; kisha apande daraja ; kwa kufahamishwa bangi na vilevi vyengine vingi na kuishilia kuwa mraibu , mzigo wa kufa mtu ; asiwe na changizo kwa wazazi wake na jamii yake kwa ujumla. Awe ameuonja unga ; sio ule wa kupikia ugali ; unga kwa jina maarufu Heroine ama vilevile Cocaine ; kichaa kimemuingia , kwao ameiba vya thamani vyote mpaka sasa ameingilia kuiba sufuria na vyombo vyengine. Wanadamu wamemsema na kumchoka kwa tabia zake zilizojaa uozo na kunuka puh! Kila mtu anamlaani . Na ujue hawa huenda mbali , kwa kutumia mihadarati hujidunga mishipa yote mwilini ; akiimaliza akabaki kuidunga mishipa ya sehemu zake za siri kwa wanaume ; kweli hupatikani shababi tena hapo ? Hudhoofika kiafya ; na kuwa mchafu kama jalala , wala kuoga hakumbuki ; yu mbioni kutafuta hela apeleke kwa pusha apate kupona. Amekuwa mtumwa wa maisha kwa hamu yake ya kukidhi andasi za dawa hizo. Yuko mwengine nae ambaye amejitumbukiza katika kina kirefu cha wizi; matamanio ya kuwa na vitu ambavyo hajavitolea jasho yamempa tiketi ya umauti pasi na kufikia idara ya uhamiaji . Cheti cha usafiri kimekuwa tairi alilochomewa na petroli ; waja wamemchoka kwa ufidhuli ; ya arobaini imetimia wameshindwa kumvumilia. Ukiwa una hili , nao wengine wamekomaa na lile. Katika dunia iliojawa maradhi ; wengine wamedumu na uzinzi na kwa bahati mbaya wamekumbana na janga la ukimwi lisilokuwa na tiba, wanaoambiwa ni waathirika ; wameanzisha kampeni ya kufa na wenzao pasi na kuwahurumia , na si vijana peke yao ; muozo wa jamii nzima na uhalisia unaotuathiri katika maisha yetu ya kila siku. Nimetamani nivae vizuri na ishi kwa starehe ; ila sina uwezo , nikavumilia ; lakini una ufahamu wa dunia ilipofikia. Wanaume wamekuwa mashoga wengine eti kisingizio ni kujitafutia ; inaumiza na kuchukiza lakini ndio uhalisia. Watoto wa kike wamewachukua baba na babu zao na kuwa wapenzi wao , watu wanauza miili yao , staha imekosekana , dunia iliochafuka , dunia ya ujana . wachache wamejishughulisha ; vijana ndio uti wa mgongo wa uchumi wa taifa lolote , wamepania kuwa kielelezo kwa wale waliopotea njia ; yuko yule aliyempiga babake kibao na shule akaisusia , aliwashinda wavyele wake lakini dunia haijamuachia. Ulidhani kuna maneno yaendayo patupu ? Asiyefunzwa na mamaye hufunzwa na ulimwengu , leo ulimwengu umemfunza kwani keshakosekewa Mara mia. Niwaombe vijana na nijiase Mimi mwenyewe kwa maana ni mmoja wao, kweli ujani ndio shamba la uzeeni , ukipanda pantosha hapa utavuna pankwisha mbeleni. Jitahidi kwa kadri ya uwezo wako , kuwa kijana ambae kupitia kwako , walio wadogo watapata muongozo mwafaka wa maisha. Jiheshimu , hakikisha jamii yako inapona kwa ajili yako, changizo zako zinaliinua taifa lako na kuifanya dunia iwe mahali bora zaidi ya ulivyoipata. Mwisho , usiwe na kikomo, katika kukimbiza azma na ndoto zako , hakuna lisilowezekana chini ya jua. Muhimu , ikimbize mishe yako yoyote ile mchakamchaka , usiwe mtu mvivu wa kungoja kupewa kila kitu, jitume na ujitengezee mazingira bora ya maisha yako.

-Omar Abdhallah.

New Love Speaks the Language I yearned For .

My love.
How I wish my heart could speak, it could tell you how many times your name is written in it. Maybe then, you would realize how much I’ve given up just to be with you.
Honey today, my ink will speak on behalf of my heart.
I know, No human is perfect, so I’m I.
There’s one thing I’ve never stopped, ever since I came into your life, I’m always trying my best to heal your wounds. Not considering I have my own.
I’m trying my best to see you smile, Even amidst my tears, but would you know?

I’m trying, just to show you how you needed to be loved..
I could try to eternity but wouldn’t be perfect still. We all have our weaknesses right?

I know I could be boring at times. Maybe I’m not as Charming as your Ex, but honey, she’s not yours anymore.

I could be the most boring thing ever in your life, but How active I turn out to be when making dua for us, is just so indescribable,
Well probably, I enjoy talking to our creator about you, more than I do to you.
Because my main focus is our, tomorrow biidhnillah.

I hope you’ll bare with my boring nature till then😭

I know you’ll compare so many aspects between me and her. She was your dream woman right?

But I just want you to know that, my love for you is incomparable.❤

I’m waiting for that time when I’ll be the only one in your mind. That time when you fully forget her, koz

I’m ever jealous everytime I try peeping into your mind.

Tell me love, what do I do to be perfect? What don’t you love in me, maybe I can adjust… I just don’t like it when you’re down, and I’m in your life, at times I feel worthless 😢

But one thing keeps me motivated.🥰 Something tells me we’re meant for each other, that thing is what makes my love for you grow each day.

I pray that Allah guides us through, may he make us perfect for each other.
*May we share that dream future together* in shaa Allah Amiin. ❤❤🤲🏻

BECOMING A REAL MAN . ( Contemporary Society).

It’s official. You are battling out life for the sake of you. If you make a breakthrough; it’s for you. Of course every woman you meet at your early life stages ; is always optimistic of who you could become. That is what keeps most of them if not all; until they come to meet reality ; that you are still in the making and not a finished product.

Their lustfullness for that ‘dream life’ manouveres their focus on you to land on a man who has transformed into a finished product and is already successful. So men , while you fall in love ; and gather these women ; put in mind ; in the end ; you stand alone. Forget the good sex ; picnics ; happy moments and tears by your lover while giving prom

ises of raising a family together .

It’s all an illusion as explained by Theodore Norman. You have to trust your mind ; set your feelings aside. Your first priority ; should be chasing your dream ; women come ; women go ; but in the end ; will you be financially stable ; will you be proud of the old man you grow into. Or you will be regretting on how you lived your youthful life because of the choices you made that you cannot go back in time to change ; and have immensely affected your present day life.

You had ladies chanting of how great you were in bed and how loud their moans were. What a playboy and a sort of Cassanova you were back in the day.I want you to be honest with yourself and start investing in your self now.
Start saving every little coin as early as your twenties. Save that money you use on betting and buying drinks to prove you are a ‘ladies man’ everytime you go to the club. Save for your future ;for that dream house and the dream family; so that ; when all is said and done ; you’ll be aging gracefully as from your fifties . Having a whole lot of fortune on your name.

Some of these girls who are milking you dry of your financial titties are only buying time and giving you sexual pleasure to lure you into believing they love you. Only to dump you for a well off man and get married because of the imaginary standards you have not met to become a husband.

So keep toiling brother ; keep hustling dawg ;Don’t give a damn about cheap nothings. Don’t fall for pot licking ; after all you can have this with the woman of your dreams ; all day every day.

But at the moment ; this is time to prioritise and build your tomorrow ; so when the curtains are down and the play has come to an end ; Your audience will be clapping their hands in acknowledgement and the adjudicators smiling saying your script topped the billboards. I know you can achieve it ; be your own motivation , pat yourself on the back ; even when you move an inch towards your dream; don’t stop making progress , in the long run ; it is
All about you.

Story Of My Life.

People mistake telling your tale as seeking sympathy and attention. Hardly do they know that every hardship we’ve been through has transformed us into the person we are today. When i had lacked money to pay for my rent; and had to transform the prayer room at Campus into my humble abode ; the whole experience was quite hectic and worsened when i succumbed to chronic pneumonia thereafter as a result of sleeping on the cold floor which has made me vulnerable to the slightest amount of cold weather ever since . The sleepless nights trying to beat the deadline for exam dates ; that saw me differ for a whole Semester for the lack of finances to clear up my school fees then .I moved from one office to another in vain or with little success; trying to reach out for a helping hand from those whom the hand of God had blessed with. One of the honourables spitted in anguish and sheer disregard when we went to seek to raise my school fees ; he said ; ‘I don’t help people .’ Seeing my mother trying to convince him otherwise and him asking her to leave was the worst and most demeaning act i had to go through persay. I held my mother back not to keep pursuing him in awry of his ego and ignorance. But what is a humanbeing ?He forgets so fast; today he/she is alive and tomorrow he has creatures feeding on his rotten body in the grave. No title ; no riches ; nothing would do good to him after he has been silenced for good by the Almighty. My graduation Ceremony at Machakos University was a point of reflection. Having to breakdown in tears the night before ; and walking to the graduation square in utter disbelief as my mother and cousin brother Seif ali mwamose looked on. For others ; it was a simple Diploma Certificate In Education Arts ( Eng/lit) for me it was a miracle by God to honour the Boy from Diani ; Kwale County. Times had been tough back then in highschool ; and unlike the teacher i have cultivated in myself ; who listens to hear ; not to judge and also empathise with my learners. They cursed me back in highschool and proved to be prophets of doom ; lamenting that nothing Good would come out of Omar Abdhallah. I did not give up even after highschool and i don’t plan to do so anytime soon. I had prayed hard and asked Allah to fulfill the purpose for living in this world. And in short strides ; Allah has kept showing me ; though you don’t have it all ; you ought to be thankful for what Allah has bestowed upon you. Thus i adopted a motto to keep pushing and being patient ; ‘Pasos Cortos ; vision Larga’ Short steps ;large vision. And His words in the Qur’an ; ‘My success does not come ; except from Allah .’ As always having Allah as my Benefactor. I have learnt to appreciate life and live easy ; and then touching the lives of others positively was the main Agenda that came through after highschool. Going to different schools both Secondary and Primary in my locality to motivate learners into performing better ; having education standards in our county being very low. It was to give back to the community ; and this over time gave birth to Ramo and Carrie Foundation ; the motto being ; To help solve world’s deepest ineiquities. E.g Poverty ; illiteracy and diseases. We reached out to the various orphanages ; having to see somebody happy and smiling and that Allah brought you as a source of inspiration and hope is the best feeling ever. You might not be rich enough to throw a state of the Art Party or live a lavish lifestyle. But if you can touch A life positively ; that is everything. In the end ; it is not the years in your life that matter; but the life in your years. Thank you so much to all well wishers and like minded affiliates who come out in masses to make this world a better place. The question is ;What do you want people to remember you for ; when you die ?-Omar Abdhallah.
(RAMO and Carrie Foundation C.E.O).

Kare Taiuya / Kale Hairudi.

Wako wapi wale mabingwa. Zamani sie weledi tulikula daku huku tunasukwa na usingizi kwelikweli. Macho tumefunga lakini ; tukishika chapati ;kama smaku ; mkono uliganda kwenye sahani ya harage la tui. Wapo wengine tamu ilizidi ; wakajichochea mkekani.🤓🤓😂😂😂😂😂
Siku ambazo hazikuwa na purukushani ; hata watoto wa kike kwa kuniangalia tu ; nilipokuwa madrassa ; walikuwa wamenitia dosari. Mbio nijiondokee kwa vishindo na uoga nisije nikaanguka kwa haya. Hawa watoto wa leo huenda wasifahamu ; mapema wamejibandika uzazi ; ama wengine ni majambazi ; eti wajukuu wa bibi ; wakali kwanza ; cha kushangaza upo wakati waliwanyonya kina mama matiti ; kama walikosa kuwa na pesa kwenye vibeti; wanahangaisha watu kwa ufidhuli na wizi.Tulijipinda ki tabia ; katu hatukuweza kumjibu mtu alietuzidi umri ; hata japo alitudhulumu tukahisi kiungulia ; tungewangoja wazazi wetu kuwaelezea ; na kiukweli ; mara nyingi watu wazima wengi walipania kuterekebisha tu ili kuboresha jamii. Japo mafidhuli hawangekosa ; tukaambiwa tuwe macho tusipewe pipi kunyamazishwa na mtu aliekua na nia mbaya. Ndani ya mwezi huu mtukufu nakumbuka kila baada ya futari kuelekea mida ya baada ya Swala ya Isha. Vijana walizunguka nyumba hadi nyingine ; wakitumbuiza watu ; Diani almaarufu tuliviita ; vigoma. Ngoma zenyewe sio kama zile za kitamaduni za kutumia ngozi kama zilivyokuwa sehemu nyingine ; ilikuwa ni kama hii mikebe ya chuma inayotumiwa kupima na kuuzia Makaa leo ; pande zote mbili ziko wazi ; kisha mikebe hio iliwambwa kwa karatasi ya Nailoni, ngumu ambayo ingehimili mikono ya masogora hawa wadogo. Basi walipofika nyumbani kwetu ; nilizifurahikia ngoma hizo ; na japo sikuwa mweledi wa kucheza nilinengua mauno kisawasawa ; nikajiingiza katika mduara , mama na baba ; wakabaki wakicheka siku hizo za jua. Ila kuna nyimbo moja iliyokuwa na kibwagizo hiki ;’Nilikuwa nae msichana wa kikamba ; nikamshika titi akasema ; watindaata ; Nesa.’🤭🤭😂😂 mpaka leo ; sijapatapo kumjua mtunzi na malengo yake . Ama ile nyimbo nyingine ; ‘ kosi n’kpwereru ; nyota zinang’ala ; lamkani mrye daku ; saaa zikafika.’ Katika lugha ya kidigo ; ilimaanisha ; ” kote ni kweupe ; nyota zinang’ara ; amkeni mle daku ; saa zimefika.” Bwana weeh ! Nyimbo tamu zilizofurahisha ujanani..Wanadensi hawa sijakwambia walikuwa wavulana wadogo na wasichana pia ; weledi wa kucheza si haba. Baada ya kucheza ; waliotumbuizwa walisema ahsante kwa kupeana pesa kidogo ; ama hata kuwakaribisha wanadensi kwa kuwapa chakula, nao wangekibeba. Basi siku hizo ; mama aliniruhusu niwafuate nyumba kadhaa zengine huku akinionya nisiende mbali sana ; lisitokee la kutokea nikamtia wasiwasi. Mama alinijali sana siku hizo ; kama anavyonijali sasa hivi , tena mwana mmoja kama roho ; angefanyaje kipenzi changu. Kisha usiku huo nilijirudia nyumbani na wenzangu tukisimulia simulizi kuhusu wanenguaji bora wa viuno wa kike ; japo hatukufahamu ungefika wakati hilo lingekuwa si jambo la kawaida tena ; kama Watoto wadogo wanavyotoa macho kuwaangalia wachezaji wa singeli leo ; walio na muozo maana hata nguo huzipunguza wakawatia hamuni waangalizi wao. Sie hatukufikia huko ;hapa Kwetu Diani.

Simulizi – kare taiuya…. itaendelea…..
#Ramadhan Kareem Wa Saum Maqbul.

Unrequitted love.

Words can not
explain the feeling.
It was heaven on earth. Now i miss every bit of it ; because i know you are not coming back.
To wake up on the same bed with you ; and looking at your face smiling before you even wake up.
Is a scene i don’t want to erase from my mind..
Then the morning kiss ; afraid you had not brushed your teeth but i was always okay with it.
The cuddling in the nights; and the height of it all ; you know what took my breathe away.
…Your love ; so tender and pure; so true and deep.
Never judging me ; always ready to sacrifice for my sake.
Your beauty;there to stop a calamity. In your arms is where i long to be once again.
To love you more; to spoil me; cause you run me ; and am okay with it.
I see you when am deep in my thoughts , they say it’s an obsession. But they are wrong. They never dined with the Royals. We know what it tasted.
You treated me like a king and adored me.
You Said i was the best thing that ever happened to you.
The love was two way; a lot of respect for one another ; hillarious moments ; romantic picnics ; and then breaking down at the thought of this whole thing crumbling.
It’s crazy how i never feel any bit of hatred for the decision you took. Maybe ; the prophecy came to pass : To love and to be loved is the greatest happiness of existence.
I yearn for you every day ; and yet i know i can never have you.
But am certain when we are no more; after death ;our souls will be in high spirits to rekindle the lost love.
They love me ; but never have they done it right ; like you did.
I really miss you.

Design a site like this with WordPress.com
Get started